Jumanne, 5 Agosti 2014

Hisia za kuumizwa katika mapenzi kwa mwanaume hazitofautiani na za mwanamke,,wote wanaumia

Katika mapenzi kwa asilimia kubwa wanawake huwa wanaona wenyewe ndiyo wanaumia sana linapotokea  suala la usaliti katika mahusiano aliyonayo, lakini ni wazi kabisa hata wanaume wanaumia sana kwahiyo usifikiri mwanamume akisalitiwa hawezi kuumia hapana kwani hata yeye ni binadamu inapotokea ametendwa basi lazima ataumia ijapokuwa maumivu yanatofautiana,, mwanamke anaweza kuonyesha wazi maumivu anayoyapata lakini mwanamume akawa anaumia moyoni huku akijionyesha usoni kuwa hajaumia kumbe anaumia sana. kwahiyo naweza kusema maumivu ya mapenzi hayaangalii mwanamume au mwanamke inategemea na wewe ulipenda kwa kiasi gani.

maumivu haya hutokana na vitu vingi ikiwemo kukosa uaminifu, kuachana au kuachika nk,,na kutokana na maumivu haya hupelekea baadhi ya watu kujuta kupenda,, kuapa kutopenda tena,,na hata kunywa sumu na kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi. Muhimu ni kuzingatia suala la mapenzi ya dhati na kuishinda tamaa,,hakuna anayependa kuumia katika mapenzi kwahiyo basi kama hupendi kuumizwa usimuumize pia mwenzio,,,kwasababu kuna wengine ni mahodari kuwaliza wenzi wao kila kukicha. Tubadilike jamani mimi naamini hakuna kinachoshindikana

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni